Jumatano 23 Aprili 2025 - 16:34
Baadhi ya viongozi wa nchi za Kiislamu hawana ujasiri hata wa mtoto mdogo wa Ghaza

Baadhi ya viongozi wa nchi za Kiislamu, siku moja watalazimika kutoa majibu. Naam, sisi tunawauliza watu wenye nidhamu za woga: Je, hamna hata ujasiri wa kiwango cha mtoto aliyesimama mbele ya kifaru huko Ghaza?

Kwa mujibu wa kitengo cha tarjama cha  Shirika la Habari la Hawza, maelfu ya watu walikusanyika katika eneo la Uskudar, Istanbul, ili kulaani mashambulizi yanayofanywa na Israel dhidi ya Ghaza, na kufanya maandamano makubwa kwa anuani ya “Ghaza inaelekea kufa, zinduka!”

Waandamanaji walipandisha bendera za Uturuki na Palestina juu huku wakapaza sauti na kusema “Israel dhalimu itaangamizwa” na “kuzingirwa kwa Ghaza ni kitendo haramu.”

Walio shiriki walionesha mshikamano wao na watu wa Ghaza, huku wazungumzaji waliwataka Waislamu wote kulaani jinai zinazofanywa na Israel dhidi ya ubinadamu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha